SHILOLE AILALAMIKIA BASATA KWA ADHABU WALIYOMPA NA KUDAI KUWA ANAWANAOMTEGEMEA WENGI

By    
Baada kufungiwa kujishughulisha na shughuli za sanaa kwa kipindi cha mwaka mmoja, mwanadada Shilole ameibuka na kuongea haya; “Mnataka nikaishi wapi nina familia ya watu 10 ndani, nina watoto 2 wanaosoma boarding kila mwaka ninatakiwa nilipe mil 5 kila mmoja, nina watoto 3 yatima ninaowalea wanasoma vilevile, kupitia muziki huu huu ninaofanya ambao watu wengine mnaudharau lakini ndio unaonifanya nifike hapa, ninalipa kodi ya nyumba Mil 7 kwa mwaka, ninalipa kodi ya maendeleo ya nchi yangu na bado nina watu ninaowasaidia”