COMMING SOON! COLLABO KATI YA DIAMOND PLATNUMZ NA NE-YO

By    

 
Akiwa nchini Afrika kusini msanii machachari sukari ya warembo, raisi wa WASAFI amepata nafasi ya kukutana na wasanii wengine wa hapa Afrika na kutoka mabara mengine ambao wako nchini Afrika ya Kusini kwa ajili ya kushuhudia na kutumbuiza katika tuzo za muziki za MTV ambazo Diamond pia ni mmoja ya washiriki. Baada ya kupiga stori na D Banj ndipo Diamond alipopewa taarifa ya kuwa anatafutwa na msanii NE-YO kutoka nchini marekani na kufanikisha kuonana nae na kupiga stori kadhaa ambazo bado hajaziweka wazi kuwa ni kipi hasa ambacho wakali hao wawili walikuwa wakiteta.