MAPINDUZI YA BONGOFLEVA, ALBAMU YA MSANII WA TANZANIA KUGHARIMU TSH. 200,000/=

By    
 
Star wa muziki Barnaba, amejinadi kuwa albamu yake mpya itaingia sokoni kwa bei ya dola 100 ama zaidi, pesa ambazo zinakadiriwa kufikia shilingi laki 2 za Tanzania kwa nakala 1.Mkali huyo amekuwa akijiamini kutokana na ubora wa nyimbo, utofauti na uwekezaji mkubwa anaoendelea kuufanya kukamilisha kazi hiyo.Barnaba ameeleza kuwa, baadhi ya rekodi kutoka albam hizo zimekwishapelekwa nchi mbalimbali ikiwepo Afrika Kusini na Ujerumani kwaajili ya 'Mastering', zikitarajiwa kutoka kwa mfumo wa DVD, na vile vile CD za kawaida, kwa bei hiyo ambayo hata hivyo amesisitiza kuwa inaweza kuongezeka zaidi.

Source: EATV