Imeandaliwa na; Steven Mwakyusa,Tumsifu Kaoza na Moringe Jonasy
Hizi ndizo nyimbo zilizofanya vizuri zaidi katika bongo flava kwa mwaka 2015
1. Nivumilie-Barakah da Prince & Ruby
2. Subira-Kassim Mganga & Christian Bella
3. Sophia-Ben Paul
4.Nashindwa- Christian Bella
5. No body but me-Vanessa Mdee &Kcee
6. Chekecha Cheketua-Alikiba
7. Na yule-Ruby
8. Game-Navy Kenzo ft Vanessa Mdee
9. Nana-Diamond & Flavour
10. Shauri zao-Belle 9
11. Nikuite nani-Jux
12. Suna-Barnaba
13. Nitazoea-Mo music
14. Nusu nusu-Joh Makini
15. For u-Q chilla
16. Shikorobo-Shetta
17. Viva Roma- ROMA
18. Safari-Nick wa pili, G nako, Joh Makini & Vanessa Mdee
19. Siri-Barnaba & Vannesa Mdee
20. Aiyola-Harmonize
Hawa wameonekana kufanya vizuri kwa mwaka unaoenda kuisha, ukiangalia
kwa makini katika hii list utagundua kwamba kuna aina ya muziki ambayo
inashika chart kwa sasa..na si nyingine bali ni Afro-pop!!
Ukimwangalia Shetta kabadilika kwa kiasi kikubwa, Q chilla naye
alionesha mabadiliko makubwa katika ngoma ya For u, huku naye Jaffarai
akijaribu kutoka katika stail yake ya zamani katika wimbo
aliomshirikisha Kassim "Wakati"...ni wengine wamejaribu kuendana na
wakati uliopo, pengine bahati haikuwa kwao!!
Ukiangalia nafasi ya Hip hop na RnB bado ni finyu, huu unaonekana kuwa
muziki ambao unapoteza mvuto kila kukicha...wasanii wengi wameshindwa
kutamba licha ya kutoa nyimbo..katika hilo kundi wamo akina Young D, Jos
Mtambo, N2N pia wasanii wa Tamaduni music!!
Wapo wasanii waliofanya vizuri mwaka uliopita lakini mwaka huu
wameshindwa kufurukuta, hawa ni pamoja na Recho, Mwasiti, Tumbulo, Rich
Mavoko, Ommy Dimpoz, MwanaFa na Ay, Madee, D knob pia Dayna Nyange kwa
kutaja kwa uchache!!
Nyota imeonekana kung'aa sana kwa Vanesa Mdee, Ruby pamoja na Christian
Bella...hawa wameweza kutengeneza hits zao...na pia kufanya vizuri pale
waliposhirikishwa!!
Mwisho niwapongeze wasanii wote walioweza kutengeneza nyimbo nzuri na
kutoa burudani ya uhakika kwa mashabiki, muziki wetu unakua japo bado
kuna zile kauli kwamba muziki ulikuwa zamani!! Leo si ajabu kuona nyimbo
zetu zikichezwa katika radio stations na Tvs za mataifa mbalimbali!
Bado naamini tunaweza kufanya vizuri zaidi ya hapa na kuitangaza vyema nchi yetu!!
Muhimu: Orodha hii imetumia maoni binafsi ya waandishi na michango mbalimbali kutoka mitandao ya kijamii.
Happy New Year 2016!!