Early life
Said Ngamba au Mzee Small (amezaliwa mw. 1955) ni msanii wa
maigizo na vichekesho kutoka nchini Tanzania. Huenda akawa anaaminika
zaidi kuwa mmoja wa wasanii wakongwe kwa nchi ya Tanzania, hasa katika
fani ya uchekeshaji ambayo sasa inachezwa zaidi na vijana.
Career
Pamoja na kuwa yeye ndiyo mwanzilishi wa kuonyesha vichekesho
kupitia luninga, lakini bado amesimama kufanya maigizo ingawaje alianza
sanaa hiyo miaka 30 iliyopita na alipata kufundishwa na Bw. Said Seif
‘Unono’ (ambaye kwa sasa ni marehemu).
Mbali na kushiriki sanaa katika vikundi mbalimbali, pia Mzee
Small amecheza sanaa katika vikundi vya mashirika kama vile Reli, NASACO
na mengine mengi, ambayo kwa sasa hayajihusishi tena na shughuli hizo.
Umaarufu
Mzee Small alianza kujulikana sana katika fani ya uchekeshaji
hasa pale alipoibuka na mchezo unaojulikana kama 50, 50, 100, na ule wa
Mjini Shule unaomwelezea mwanamke mmoja wa kijijini aliyeolewa mjini.
Mbali na kutamba na michezo hiyo, Mzee Small pia ni mcheshi na
mwenye kupenda utani wakati wote, aliibuka na kichekesho kisemacho Nani
Mwenye Haki, ambacho sasa ameamua kukiboresha zaidi.
Pia ameibuka na kitu kingine kiitwacho “Nani Kama Shule" huku
akiwa amewashirikisha wakina Majuto, Kingwendu nawachekeshaji wengine
wanaotamba sasa nchini Tanzania.
Kundi binafsi na usanii wake
Mzee Small anamiliki kundi lake la sanaa linalojulikana kama
Afro Dance ambalo alilisajili mwaka 1994 kwenye Baraza la Sanaa la
Taifa, BASATA, na kupata usajili rasmi mwaka huohuo wa 1994.
Pamoja na kuwa na uzoefu wa kisanaa, lakini bado hana mpango
wowote ule wa kujiunga na kundi jingine, ila anachoweza kufanya ni
kurekodi na wasanii wengine atakapoitwa kwa makubaliano maalum. Mzee
Small alisema:
“Sina mpango wa kujiunga na kundi jingine wakati mimi nina kundi
langu la Afro Dance, kama mtu au kikundi kinanihitaji ninachoweza
kufanya ni kurekodi nao kwa makubaliano maalum, lakini sio kuchukuliwa
kabisa na kundi hilo, “alisema Mzee Small”
Alisema kuwa kwa sasa anajitahidi kuboresha kazi yake na
kuzisimamia katika mauzo, na wakati hana shughuli nyingi hujishikiza
katika duka moja Kariakoo la Home Shopping Centre.
Maisha binafsi
Akizungumzia mafanikio aliyopata kutokana na vichekesho, Mzee
Small alisema kwa utani “nimempata mke wandoa katika televisheni ambaye
ni Bi. Chau.” Small akaeleza:
“Bi. Chau ni mke wangu wa ndoa katika televisheni na hakuna mtu
anayempenda mkewe au mpenzi wake kama mimi na Bi. Chau tunavyopendana,
kama wapo ni vizuri zaidi, “alisema Mzee Small.
Alisema kuwa mkewe, Bi. Fatuma hana tatizo lolote na Bi. Chau
kwani anajua nini ninachofanya, hii ni kazi kama nyingine hivyo
analielewa hilo.”
Akizungumzia kikweli kweli mafanikio yake yaliyotokana na
uchekeshaji, Mzee Small alisema kuwa kwa sasa anaishi kwake na hana
ugomvi na baba wala mama mwenye nyumba, “hilo kwangu halipo kwa sasa.”
“Mbali na kuishi kwangu, pia naendelea kupata mkate wangu wa
kila siku na ninaweza kuwasomesha watoto wangu, mmoja yuko kidato cha
tano, mwingine sekondari ya kawaida na wengine shule ya msingi, kwa pesa
hii hii ya vichekesho, “alisema msanii huyo.
Mzee Small kwa sasa ana watoto watano, watatu wakiume na wawili
wakike, ambapo anawasisitizia watoto wake kusoma na kama wanataka
kujiingiza katika sanaa, “huo utakuwa ni uamuzi wao baada ya kumaliza
masomo.”
Ugonjwa
Mzee Small alipata matatizo ya ugonjwa wa kiharusi mnamo
September mwaka Jana na mpaka sasa akiendelea na matibabu ya ugonjwa huo
chini ya uangalizi wa familia yake na pia kutokana na michango ya watu
wenye mapenzi mema kwake.
Ushauri wake na sifa kwa wasanii wengine wa Tanzania
Mzee Small aliotoa ushauri wake kwa wasanii chipukizi wanaoibuka,
Mzee Small aliwataka kutobweteka na kubuni vitu vipya kila wakati ili
vichekesho au maigizo yao yapendwe kila kukicha, sio kuridhika na
walipofikia.
Pia aliwasifu akina Bambo, Kingwendu na wachekeshaji wengi ambao
alisema wameonyesha vipaji vikubwa, “lakini sasa kinachotakiwa ni kwa
mara kwa mara kubuni mbinu mpya ya uchekeshaji au uigizaji.
MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALA PEMA PEPONI, AMEN.