Je waujua utamu wa muziki wa kitanzania, basi huyu ndiye jamaa anayeleta utamu wa muziki huu wa RNB Bongo. Jamaa ana nyimbo nyingi sana kali kama maneno, samboira, nikikupata, anaishi naye, pete n.k ambazo zimemtambulisha kwenye gemu ya bongofleva na kumpa TUZO kibao. Icheki video yake ya jikubali mwenyewe uikubali.
Pale mtu anapofanya vizuri hatuna budi kumpa hongera kwa kile alichokifanya, nami vile vile sina budi kumpa hongera mwanadada ambaye kila siku tumezoea kumuona katika tasnia ya filamu na sasa kaamua kuingia kunako muziki. Kwa upande wangu ngoma ni kali sana kwa mashairi, mdundo hadi sauti. Isikilize na kujionea mwenyewe upate ladha yake